14 August 2013

Vigogo wahusishwa na ujangili

MWENYEKITI wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, James Lembeli, amesema kuna kila dalili kwamba baadhi ya vigogo serikalini wanahusika na biashara ya meno ya tembo nchini.





Matukio ya watu kukamatwa na meno ya tembo nchini yameongezeka siku hadi siku kwa kuwa Julai 29, mwaka huu, watu tisa walikamatwa na meno ya tembo, wawili kati yao wakiwa polisi wa Kituo cha Oysterbay, Dar es Salaam waliokamatwa Kisarawe, mkoani Pwani, wakisafirisha meno 70 ya tembo (kilo 305) kinyume cha sheria.


Lembeli aliyasema hayo katika kikao cha pamoja kati ya kamati yake na watendaji wa Wizara ya Maliasili na Utalii jijini jana na kusema kuwa meno hayo kwa hesabu za kawaida ni sawa na tembo 35, thamani yake ni zaidi ya sh milioni 850, huku juzi raia wa Uingereza Robert Dewar akikamatwa nchini akiwa na nyara za serikali zenye thamani ya sh 118,314900.


Raia huyo ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Trans Afrikas Longistics (TALL) alikamatwa na vipande nane vya meno ya tembo, vinyago 11, meno 20 ya tembo, meno 20 ya simba, kucha 22 za simba, ndege mmoja aina ya kasuku, vipande vya miti ya mpingo na idadi kubwa ya vinyago vitu vyote hivyo vilikuwa na uzito wa kilogramu 24, alivyokuwa navyo kinyume na sheria.


Lembeli alisema kuwa hatua ya kuendelea kwa matukio ya kuuawa kwa tembo nchini inatoa ishara kuwa serikali haina haja ya kuchukua hatua kwa sababu inafanywa na watu wakubwa.




Source;  Tanzania Daima



Sijui tutafikaje???

No comments:

Post a Comment