16 May 2013

ALIISHI KWA SIKU 17 AKILA BISCUIT NA MAJI


DHAKA, Bangladesh Msichana aliyenusurika baada ya kuishi kwa siku 17 chini ya kifusi cha ghorofa lililoporomoka mjini Dhaka, Bangladesh, amesema biskuti alizonunua kwa ajili ya kifungua kinywa akiwa kazini ndizo zilimnusuru kufa kwa njaa.
Reshma Begum aliishangaza dunia baada ya kuokolewa chini ya kifusi cha jengo hilo, lililoporomoka Aprili 24, mwaka huu na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 1,000.watu zaidi ya 2,500 waliokolewa kati ya watu zaidi ya 3,000 ambao walikuwa wakifanya kazi ndani ya jengo hilo la ghorofa nane.
Msichana huyo ambaye hakuwa na majeraha ya kuhatarisha maisha yake, alisimulia mkasa wake kwamba aliishi kwa kula biskuti na kunywa maji ya chupa yaliyodondoka kwenye eneo lake, bila kufahamu yalikotoka.
Reshma (19) alisema siku ya ajali hiyo, aliamka asubuhi kuwahi kazini bila kupata kifungua kinywa ambapo akiwa njiani alinunua mabunda madogo manne ya biskuti ambazo angekula kabla ya kuanza kazi.

sOURCE: MWANANCHI




No comments:

Post a Comment