27 October 2012

Mmmmmh!



Mwanza
Siku moja baada ya Jeshi la Polisi kutoa taarifa ya awali ya uchunguzi wa mauaji ya kifo cha aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Liberatus Barlow, ujumbe mfupi wa simu ya mkononi kwa ajili ya kutekeleza mauaji hayo imenaswa.
Kamanda Barlow aliuawa usiku wa manane alipokuwa akitoka kwenye kikao cha harusi ya ndugu yake. Alifikwa na mauti hayo baada ya kupigwa risasi akimsindikiza Mwalimu Doroth Moses.


Habari zilizopatikana kutoka kwa baadhi ya makachero jijini Mwanza zinaeleza kuwa, ukweli wa mauaji hayo umebainika na kwamba watuhumiwa waliokamatwa wanahusika moja kwa moja na mpango kamili wa mauaji hayo.
Kupatikana kwa wauaji hao, kumetokana na simu ya Mwalimu Dorothy Moses kupitia ujumbe wa simu aliokuwa akiwasiliana na wahusika.


Source: Mwananchi; 27/10/12

No comments:

Post a Comment